Monday, October 27, 2014
MTIBWA KILELENI MWAMBUSI APEWA ULINZI
Do you like this story?
Kocha msaidizi wa Timu ya Mbeya City Suleiman Jabir akimtoa nje Mchezaji Paul Nonga mara baada ya mchezo kuisha |
Kikosi cha Timu ya Mtibwa |
Kikosi cha Timu ya Mbeya City |
Mashabiki wa Mbeya City wakikimbia mara baada ya kuanzisha fujo uwanjani |
TIMU ya Mtibwa ya mjini Morogoro imeifundisha kabumbu timu ya Mbeya City
kwa kuilambisha jumla ya magoli 2-0 katika uwanja wa kumbukumbu ya Sokoine
Jijini Mbeya.
Mbeya City ambayo imepoteza mechi ya pili katika uwanja wa nyumbani baada
ya wiki iliyopita kufungwa na Azam 1-0, ilishindwa kuutawala mpira katika
dakika zote za mchezo.
Mpira ulianza kwa kasi huku kila timu ikijitahidi kusaka bao lakini
dakika ya 21 ya mchezo mpira wa kona uliopigwa na David Luhende na kumkuta Amri
Ally aliyeutingisha wavu wa Mbeya City.
Hadi kipindi cha kwanza kinamalizika Mbeya City walikuwa nyuma kwa bao
1-0.
Kipindi cha pili kama ilivyokuwa katika kipindhi cha kwanza timu
zilishambuliana kwa zamu huku, Mtibwa wakilihami goli lao na kutaka kuongeza
bao nao Mbeya City wakijitahidi kulishambulia lango la Mtibwa bila mafanikio.
Kila timu ilifanya mabadiliko katika kipindi cha pili ambapo kwa upande
wa Mtibwa Mussa Mgosi alitoka na nafasi yake kuchukuliwa na Vicent Barnabas
ilhali Mbeya City ilimtoa Saad Kipanga na nafasi yake kuchukuliwa na Mwagane
Yeya.
Mabadiliko hayo ya kila timu yalibadilisha kidogo hali ya mchezo ambapo
ari na nguvu mpya ya mpira ilianza kuonekana kwa kila upande.
Hata hivyo ilikuwa ni dakika ya 78 ya mchezo mchezaji wa Mtibwa
aliyeingia kipindi cha pili Vicent Barnabas aliwainua wapenzi wake kwa
kuifungia Mtibwa bao la pili na kuzua kizaazaa kwa upande wa mashabiki wa Mbeya
City ambao walianza kuwarushia mawe na chupa za maji wachezaji wa Mtibwa ambao
walikuwa wakishangilia bao hilo.
Hali hiyo ilisababisha kikosi cha kutuliza ghasia kuwasha gari lake la
washawasha na kutoa alama ya tahadhari kwa kupiga honi na king'ora.
Jukwaa la mashabiki wa Mbeya City lilibaki wazi huku hamasa za
kushangilia zikipungua ilhali ndani ya uwanja wachezaji wa Mbeya City
walionekana kupanic kwa kucheza mpira wa piga nikupige huku wenzao wa Mtibwa
wakituliza mpira chini.
Hadi kipyenga cha mwisho Mtibwa walikuwa wakiongoza kwa bao 2-0 ambapo
mashabiki wa timu ya Mbeya City walionekana kutoamini matokeo hayo huku
wachezaji wa Mbeya City wakitahayari na kuendelea kubaki katikati ya uwanja.
Katika hatua nyingine wachezaji wa Mbeya City walisusia kupanda gari lao
na kutembea kwa miguu kutoka nje ya uwanja kuelekea kambini katika hoteli ya
Holiday iliyopo jirani na uwanja huo. Mashabiki wa timu hiyo walisikika
wakimlaani wazi wazi kocha wao Juma Mwambusi na kusema kuwa hawamtaki kwa kuwa
ameshindwa kuifundisha timu hiyo.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “MTIBWA KILELENI MWAMBUSI APEWA ULINZI”
Post a Comment