Monday, November 3, 2014
BARACK NA MICHELLE OBAMA WADAIWA KULUMBANA TENA, KISA MWANAMKE.
Do you like this story?
Kwa
mujibu wa habari zinazoandikwa kwenye mitandao ya nchini Marekani, Michelle
Obama anadaiwa kumfukuza mumewe Barack Obama nje ya ikulu ya White House baada
ya kudaiwa kumchombeza mwanamke aliyechumbiwa wakati wakipiga kura huko Chicago
hivi karibuni
Tukio
hilo lililomhusisha msichana aitwaye Aia Cooper, liliandikwa sana na vyombo vya
habari kama jambo la utani tu kwakuwa Obama alikuwa akimtania msichana huyo
pamoja na mpenzi wake.
Tukio hilo
lililomhusisha msichana aitwaye Aia Cooper, liliandikwa sana na vyombo vya
habari kama jambo la utani tu kwakuwa Obama alikuwa akimtania msichana huyo
pamoja na mpenzi wake.
Katika tukio hilo,
mchumba wa Cooper alipita karibu na Rais Obama wakati akiwa kwenye chumba cha
kupiga kura ambako Aia alikuwa akipiga yake pia na kumwambia “don’t touch my
girlfriend.”
Obama alisikika akisema: There’s an example of a brother just embarrassing me for no reason, just for no reason whatsoever.”
Kwa wengi, jambo hilo
liliishia hapo lakini kwa mujibu wa ripoti za hivi karibuni Michelle
hakufurahishwa nalo hata kama lilikuwa la utani. Inadaiwa kuwa baada ya
Michelle Obama kuona video hiyo alichukia.
Chanzo kimoja
kimesema: The way it’s going, Barack
may be living elsewhere by the time his second term ends. Michelle’s about to
kick him out for good!”
Hii si mara ya kwanza
Michelle anadaiwa kuchukia baada ya mumewe kuonesha uchombezaji kwa mwanamke
mwingine. Mwaka jana kwenye mazishi ya Mandela, Michelle alidaiwa kuchukizwa na
kitendo cha mume wake kuwa karibu mno na waziri mkuu wa Denmark Helle
Thorning-Schmidt ambako walipiga selfie pamoja na waziri mkuu wa Uingereza,
David Cameron.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “BARACK NA MICHELLE OBAMA WADAIWA KULUMBANA TENA, KISA MWANAMKE.”
Post a Comment