Monday, January 4, 2016

HALL HANA MPANGO NA MAPINDUZI CUP ZAIDI YA KUTALII TU ZENJ


Stewart Hall (kulia) kocha mkuu wa timu ya Azam FC


Kweli ukisema cha nini wenzio wanasema watakipata lini, hivi ndivyo unaweza kuichukulia kauli iliyotolewa na kocha mkuu wa Azam FC Stewart John Hall juu ya michuano ya Mapinduzi Cup inayoendelea visiwani Zanzibar.

Raia huyo wa England amesema michuano ya Mapinduzi kwake si lolote si chochote ndiyo maana amewapumzisha wachezaji wake wengi wa kikosi ambacho kimezoeleka kuanza na kuwapa nafasi wachezaji ambao wamekuwa hawana nafasi kubwa kwenye timu hiyo.

Hall amesema kombe la Mapinduzi kwake sio kitu wala halipo kwenye mipango yake badala yake akasema mataji yanayomuumiza kichwa ni ligi ya Vodacom Tanzania bara, kombe la FA (Azam Sports Federationa Cup) pamoja na kombe la shirikisho barani Afrika.

“Tumejiandaa kwa ajili ya Vodacom Premier League, Azam Sports Federation Cup (FA) pamoja na Confederation Cup lakini siyo Mapinduzi na hiyo imepelekea kubadili wacheaji 10 na kama kuna wa kulaumiwa basi ni mimi lakini siyo wachezaji”, amesema Hall ambaye anaonekana hana mpango kabisa na michuano ya Mapinduzi.

“Michael Balou amekwenda kwao kwenye msiba, Agrey Morris, Kapombe na Erasto Nyoni wao ni majeruhi, Farid Mussa anaenda Ulaya na nikaamua kumpumzisha Wawa kwasababu anatumika sana karibu kwenye kila mechi”.

Mchezo wa Azam FC vs Mtibwa Sugar, Hall aliwaanzisha kwenye benchi Ivo Mapunda, Jean Mugiraneza, Kipre Tchethe, John Bocco, Frank Domayo ambao wengi wao mara nyingi wamezoeleka kuonekana kwenye kikosi cha kwanza cha timu hiyo.

0 Responses to “HALL HANA MPANGO NA MAPINDUZI CUP ZAIDI YA KUTALII TU ZENJ”

Post a Comment

More to Read