Sunday, October 30, 2016

BARAZA LA MADIWANI MAKETE LAWAFUKUZA KAZI WATUMISHI 9




Baraza la Madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Makete mkoani Njombe baada ya kujigeuza kama kamati, wameridhia kuwafukuza kazi watumishi wa halmashauri hiyo kutokana na makosa mbalimbali waliyoyatenda

Akitangaza uamuzi huo katika baraza la Madiwani hapo jana, Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo Mh. Egnatio Mtawa amesema jumla ya watumishi 13 wamejadiliwa, 9 kati yao wamefukuzwa kazi huku wengine wakichukuliwa hatua nyinginezo ikiwemo kushushwa cheo

Hata hivyo kupitia baraza hilo wapo watumishi wengine waliowajibishwa kwa kuondolewa majukumu yao ili kupisha uchunguzi kutokana na Mchakato wa uvunaji wa msitu wa Iwawa na Nungu kufuatia  kasoro zilizojitokeza huku Mkurugenzi akiagizwa kuunda timu ya uchunguzi wa suala hilo ambayo itatakiwa kuleta taarifa yake rasmi baada ya miezi miwili kuanzia oktoba 28


Aidha madiwani hao pia wamewathibitisha kazini jumla ya watumishi na msisitizo kutolewa kwao kuwa wafanye kazi zao kama serikali ya awamu ya 5 inavyotaka

0 Responses to “ BARAZA LA MADIWANI MAKETE LAWAFUKUZA KAZI WATUMISHI 9”

Post a Comment

More to Read