Saturday, November 5, 2016
BODI YA MIKOPO ELIMU YA JUU YAANZA KUWAPA WANAFUNZI FEDHA ZAO IFIKAPO LEO
Do you like this story?
Bodi
ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HELSB), imeagizwa kuhakikisha kuwa fedha zote
zilizotengwa kwa ajili ya mikopo ya wanafunzi wanaoendelea na masomo
zinapelekwa vyuoni ifikapo leo.
Agizo
hilo lilitolewa bungeni jana na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi,
Profesa Joyce Ndalichako baada ya wabunge mbalimbali kuomba miongozo kwa Spika
kuhusu kuwapo kwa wanafunzi wengi waliokosa mikopo kwa mwaka wa fedha 2016/17.
Mwongozo
kwa Spika ulitiliwa mkazo na Mbunge wa Chalinze (CCM), Ridhiwan Kikwete
aliyeeleza kuwapo taarifa kutoka Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM) kuwa
wanafunzi wanataka kugoma kwa kukosa fedha za mikopo.
Kutokana na miongozo hiyo, Mwenyekiti wa Bunge, Najma Giga aliitaka Serikali kutoa maelezo.
Kutokana na miongozo hiyo, Mwenyekiti wa Bunge, Najma Giga aliitaka Serikali kutoa maelezo.
Akitoa
kauli ya Serikali, Profesa Ndalichako alisema fedha za mikopo kwa ajili ya
wanafunzi zilikwenda vyuoni wiki moja iliyopita.
“Tatizo
lililotokea kwa UDSM sijui kama walidanganyana au la lakini hawakujaza fomu.
Serikali haitatoa mkopo kwa mwanafunzi ambaye hajajaza fomu. Na waliosaini leo
wataingiziwa fedha zao kwenye akaunti na vyuo,”alisema.
Kuhusu
wanaoendelea na masomo, Profesa Ndalichako alisema wanafunzi wote wanufaika na
wanaoendelea na masomo wataendelea kupatiwa mikopo kama ilivyokuwa mwaka
uliopita.
Alisema
wanafunzi ambao vyuo vyao vimewasilisha HELSB taarifa za matokeo, Bodi
imekwishawatumia fedha vyuoni kwa ajili ya kuwapa mikopo wanafunzi hao.
Hata
hivyo, alisema taratibu za kuwabaini wanafunzi wenye sifa zinaendelea na wasio
na sifa wataendelea kuondolewa kupata mikopo.
Pia,
alikiri kuwa ucheleweshaji wa matokeo ya wanafunzi wanaoendelea na masomo
umeathiri kasi ya kutuma fedha vyuoni.
“Wizara
yangu imekwishaagiza vyuo vyote ambavyo havijawasilisha matokeo ya mitihani ya
wanafunzi wao kwa mwaka wa masomo uliopita, kufanya hivyo mara moja,”alisema.
Ndalichako
alisema hadi kufikia Novemba 3 mwaka huu, Sh71.042 bilioni zilikwishatumwa
vyuoni kwa ajili ya wanafunzi wa mwaka wa kwanza na wanaoendelea na masomo.
Akizungumzia
utoaji wa mikopo kwa mwaka wa fedha 2016/17, Ndalichako alisema katika mwaka
huo, Sh483 bilioni zimetengwa na zimelenga kutoa mikopo kwa wanafunzi 119,012,
wanafunzi 93,295 wanaoendelea na masomo na wa mwaka wa kwanza 25,717.
Ndalichako
alisema katika mwaka wa fedha 2016/17 wanafunzi 58,010 walidahiliwa na Tume ya
Vyuo Vikuu (TCU) na orodha yao iliwasilishwa HELSB na hadi Novemba 2, mwaka
huu, wanafunzi 21,190 wa mwaka wa kwanza wamepewa fedha. Kati yao 4,321 ni
yatima, 118 wenye ulemavu na 87 ni waliosoma sekondari kwa ufadhili wa taasisi
mbalimbali.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
.gif)


0 Responses to “ BODI YA MIKOPO ELIMU YA JUU YAANZA KUWAPA WANAFUNZI FEDHA ZAO IFIKAPO LEO”
Post a Comment