Wednesday, April 5, 2017

KITILA,SEMAKAFU WALA KIAPO MBELE YA JPM


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli leo amewaapisha viongozi aliowateua kushika nyadhifa mbalimbali.
Rais John Pombe Magufuli akimwapisha Prof. Kitilia Alexander Mkumbo kuwa katibu Mkuu Wizara ya Maji na Umwagiliaji Ikulu jijini Dar es salaam April 5,2017

Hafla ya kuapishwa viongozi hao imefanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Mhe. Dkt. Magufuli amemuapishwa Dkt. Leonard Douglas Akwilapo kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.
Prof. Kitila Alexander Mkumbo ameapishwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Maji na Umwagiliaji.
Dkt. Ave Maria Emilius Semakafu ameapishwa kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia.
Mhe. Baraka Haran Luvanda ameapishwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini India.
Mhe. Sylvester Mwakinyuke Ambokile ameapishwa kuwa Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini.
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akimwapisha Dkt. Ave Maria Semakafu kuwa Naibu katibu Mkuu Wizara ya Elimu,Sayansi na Teknolojia Ikulu jijini Dar es salaam April 5,2017
Bw. Charles Edward Kichere ameapishwa kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
Aidha, Viongozi hao wamekula kiapo cha uadilifu kwa viongozi wa umma kilichoongozwa na Katibu wa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma Bw. Waziri Yahaya Kipacha.
Akizungumza baada ya kuapishwa kwa viongozi hao, Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan amewapongeza kwa kuteuliwa kushika nyadhifa hizo na amewataka kufanya kazi kwa kutanguliza maslai ya Taifa na kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa.
“Tutawapa ushirikiano wote mtakaouhitaji ili kufanikisha kazi zenu lakini na nyinyi msituangushe, Bw. Kichere tunakutegemea ukaimarishe ukusanyaji wa mapato pale TRA na pia ukawaambie maafisa wako na mameneja wa mikoa waache kutoa kauli za kuigombanisha Serikali na wafanyabiashara, wakusanye kodi kwa kufuata sheria na taratibu na pia wawe na lugha nzuri.
“Prof. Kitila Mkumbo tunategemea utaongeza msukumo kutatua matatizo ya maji, utasaidia kufanikisha kampeni ya kumtua Mama ndoo ya maji, Watanzania wapate maji safi na salama”
amesema Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muunganoi wa Tanzani Mhe. Samia Hassan Suluhu, Katibu Mkuu Kiongozi Balozi John Kijazi katika picha ya pamoja na Kamshna wa Mamlaka ya Mapato Tanzania TRA Charles Edward Kichele, Balozi wa Tanzania nchini Idia Baraka Luvanda, Balozi wa Tanzania nchini Afrika Kusini Sylvester Ambokile Mwakinyuke, Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Sayansi na Teknolojia Ave Maria Semakafu, Katibu Mkuu wa wizara ya Maji na Umwagiliaji Prof. Kitilia Alexander Mkumbo na Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia mara baada ya kuapishwa na Rais Ikulu Jijini Dar es salaam April 5,2017

0 Responses to “KITILA,SEMAKAFU WALA KIAPO MBELE YA JPM”

Post a Comment

More to Read