Tuesday, March 18, 2014
ATC KUANZISHA SAFARI MBEYA- DAR.
Do you like this story?
Shirika la ndege Tanzania
(ATC) linatarajia kuanza safari zake kati ya mbeya na dare s salaam
kuanzia leo likitumia ndege ya kisasa ya
CRJ – 2200 yenye uwezo wa kubeba abiria 50.
Meneja wa ATC Mkoa wa
mbeya shabani mtambalike amesema ATC itazindua huduma zake leo katika uwanja wa
kimataifa wa songwe na kwamba itafanya
safari zake mara nne kwa wiki.
Amesema matarajio yake ya
baadaye ni kuwa na safari kwa siku zote za wiki na hatimaye kuanza safari za
nchi jirani za Malawi , Zambia na
jamhuri ya kidemokrasia ya watu wa kongo(DRC).
Mtambalike amesema ATC kwa
sasa inamilikiwa na serikali kwa asilimia 100 na kuwa ndege hiyo ya CRJ-2200
inatumia injini ya jeti hivyo inao uwezo mkubwa na itakuwa inatumia muda wa saa moja kutoka dar es salaam kufika mbeya
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ATC KUANZISHA SAFARI MBEYA- DAR.”
Post a Comment