Tuesday, March 18, 2014
IDARA YA MAJI WILAYA YA MAKETE YAJIPANGA KUTOA MAJI MAKETE MJINI KWA ASILIMIA 100 IFIKAPO MEI MWAKA HUU.
Do you like this story?
Idara
ya maji wilayani Makete mkoani Njombe imejipanga kuhakikisha wakazi wa Makete
mjini watapata maji kwa asilimia mia moja ifikapo Mei mwaka huu
Kauli
hiyo imetolewa na Meneja wa mamlaka ya maji Makete mjini Bw. Yonasi Ndomba
wakati akizungumza na mtandao huu katika wiki hii ya kuelekea kilele cha siku
ya Maji duniani ambacho kwa mkoa wa Njombe kitaadhimishwa katika wilaya ya
Makete katika viwanja vya mabehewani
Bw.
Ndomba amesema kwa sasa ni asilimia 4 tu ya wakazi wa Makete mjini hawapati
maji saa 24, hivyo kutokana na mikakati wanayeoendelea kuitekeleza kwa sasa,
wanaimani hadi kufikia mwezi Mei mwaka huu maji makete mjini yatapatikana kwa
asilimia mia moja
Akizungumzia
kilele cha wiki ya maji, amesema kimkoa maadhimisho yatafanyika wilayani hapa
na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa mkuu wa mkoa wa Njombe Kapteni mstaafu Aseri
Msangi, ambapo amewataka wananchi kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho hayo
Mkuu
wa mkoa anatarajiwa kuweka jiwe la msingi ujenzi wa tanki la maji lililopo
Mwongolo, Makete mjini pamoja na mkutano wa hadhara utakaofanyika katika
viwanja vya mabehewani pamoja na burudani mbalimbali kutoka kwenye vikundi vya
sanaa vilivyopo wilayani hapo
Kwa
upande wake Kaimu mhandisi wa maji wilaya ya Makete Bw. Nahom Tweve ametoa wito
kwa wananchi kuacha tabia ya kuchunga mifugo kwenye vyanzo vya maji kwani kwa
kufanya hivyo kunasababisha maji kuzidi kupungua wilayani hapo, hivyo adha ya
maji itazidi kuongezeka badala ya kupungua
Amesema
kwa kuwa sheria zipo, yeyote atakayekamatwa na serikali akiharibu vyanzo vya
maji atachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria ili iwe fundisho kwa wengine wenye
tabia kama hiyo
"Miaka
30 iliyopita ndani ya wilaya hii kuna mito ilikuwa huwezi kuvuka kutokana na
wingi wa maji, wapo wazee waliokuwepo enzi hizo watakuwa ni mashaidi, lakini
kwa sasa mito hiyo unajivukia biala wasiwasi kwa kuwa maji yamepungua
sana" amesema Tweve
Kaimu
huyo amesema ni lazima kila mmoja wetu atunze vyanzo vya maji kwa manufaa ya
vizazi vilivyopo na vijavyo, kwa kuacha kuchunga mifugo kwenye vyanzo vya maji,
kupanda miti ambayo ni rafiki na vyanzo vya maji pamoja na kuacha uharibifu
wowote ule kuhusu vyanzo vya maji
Kauli
mbiu ya maadhimisho ya mwaka huu ni "uhakika wa maji na nishati"
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “IDARA YA MAJI WILAYA YA MAKETE YAJIPANGA KUTOA MAJI MAKETE MJINI KWA ASILIMIA 100 IFIKAPO MEI MWAKA HUU.”
Post a Comment