Wednesday, March 19, 2014
WANAFUNZI WAMKATA PANGA MWALIMU WAO.
Do you like this story?
Wanafunzi wawili wa
shule ya sekondari ya kibara, wilayani
bunda wamefikishwa mbele ya mahakama ya hakimu mkazi wa bunda wakikabiliwa na shtaka l a kumshambulia na kumjeruhi kwa
panga mwalimu mkuu wa shule hiyo.
Ilielezwa kuwa wanfafunzi hao walimjeruhi mwalimu huyo
baada ya kutaka kurejeshewa fedha zao za ada kwa vile hawakuwa na mpango tena wa kuendelea na masomo shuleni hapo.
Hata h ivyo imeelezwa
kuwa kuna uongozi wa shule hiyo ulipnga azma hiyo ya wanafunzi kuacha shule na kurejeshewa fedha zao.
Mwendesha mashataka
mkaguzi msaidizi wa polisi masoud Mohamed aliwataja washtakiwa hao wanaosoma kidato cha tatu kuwa ni amosi
shirima (22) na james athuman (22)
Washtakiwa kwa pamoja
wanadaiwa kutenda kosa hilo machi 17 mwaka huu.
Mohammed alidai kuwa siku
ya tukio saa 5:00 asubuhi
washtakiwa hao kwa pmoja
walimvamia mkuu wa shule aliyotajwa kwa
jina la awadh said wakati akiwa ofisini
kwake shuleni hapo.
Baada ya kuvamia ofisini
kwake watuhumiwa walimshambulia sehemu
mbali mbali za mwili kwa panga na
kusababisha majeraha makubwa.
Masoud alisema baada ya
wmalimu kuona ashambulia alipiga kelele
za kuomba msaada kabla ya watu kujitokeza na kuwakamata
watuhumiwa na baadaye kuwapeleka kituo cha polisi .
Washtakiwa kwa pamoja wamekana shtaka lao mbele ya
hakimu mkazi mfawidhi wa mahakama hiyo safina semfukwe.
Hakimu semfukwe aliamuru
washtakiwa kurudishwa rumande mpaka kesi
yao itakapotajwa april mosi 2014.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “WANAFUNZI WAMKATA PANGA MWALIMU WAO.”
Post a Comment