Thursday, October 23, 2014
KAMPUNI YA JAGRO ENTERPRISESS YAKAMATA GARI YA TAASISI YA KIBENKI NMB TAWI LA MBEYA.
Do you like this story?
Gari ya Nmb ambayo imekamatwa |
Mwana Sheria wa Kampuni ya Jagro Enterprises Bw Aloyce Mrema akitolea maelezo juu ya kukamatwa kwa Gari hilo |
Mkurugenzi wa Jagro Enterprisess Bw Maulid Hamis akimtolea ufafanuzi Mwanasheria juu ya ukamatwaji wa Gari hilo la Nmb |
Gari ya Kampuni ya Vodacom ikiwa kwenye Eneo la maegesho ya Kampuni ya Jagro mara baada ya kulikamata |
MAHAKAMA ya Wilaya ya Chunya,
Mkoani Mbeya, imetoa kibali cha kukamatwa na kuuzwa kwa
magari matatu ya Taasisi ya Kibenki ya NMB na Kampuni ya
mawasiliano Vodacom Tanzania, ili kulipa fidia ya shilingi milioni 86,553,700
kwa kosa la kumsababishia mteja hasara baada ya kuhamisha fedha kwenye akaunti
kwa kutumia huduma ya kibenki ya njia ya simu bila idhini
yake.
Kesi hiyo namba 4 imefunguliwa
mahakamani hapo, Mei 13 mwaka huu na mlalamikaji Mwanswa Jonas dhidi ya Taasisi
ya kibenki ya NMB na kampuni ya Vodacom Tanzania na mahakama hiyo kutoa
hukumu Oktoba 13 mwaka huu kwa kutoa kibali cha kuuzwa kwa magari hayo.
Akisoma shitaka hilo, hivi
karibuni, Kalani wa mahakama ya Wilaya ya Chunya Izza Sheumu, mbele ya hakimu
wa Wilaya, Desdery Magezi, alisema, Mei 13,2014 , mlalamikaji alibaini kupotea
kwa fedha zake zikiwa na thamani ya shilingi milioni 6,553,700 zilizokuwa
kwenye akaunti namba 6071600335 kupitia benki ya NMB.
Amesema, uchunguzi ulibaini kuwa
fedha hizo zilipotea baada ya kuhamishwa kwa kutumia huduma ya kibenki ya njia
ya simu kutoka akaunti namba 6071600335 kwenda kwenye namba ya
simu ya mkononi ya Vodocom 0768 713668 bila ya idhini ya mteja.
Amesema, imeelezwa kuwa wakati
zoezi hilo linafanyika mteja huyo alisitishiwa huduma ya mawasiliano kwa muda
na kwamba alipofuatilia kwenye ofisi za Vodacom, alielezwa kwamba asubiri
huduma yake itarudishwa kwani kunamatatizo ya kiufundi.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “KAMPUNI YA JAGRO ENTERPRISESS YAKAMATA GARI YA TAASISI YA KIBENKI NMB TAWI LA MBEYA.”
Post a Comment