Friday, October 3, 2014
PINDA ATAMANI KURA KABLA YA UCHAGUZI MKUU .
Do you like this story?
WAZIRI Mkuu, Mizengo
Pinda amesema ana shauku kuona Katiba Inayopendekezwa, inapigiwa kura na
Watanzania na kuwa Katiba kabla hata ya Uchaguzi Mkuu wa mwakani, kwa kuwa
ikiachiwa kuna watu wanaweza kuleta vurugu.
Alisema kazi
iliyobakia ni kupeleka Katiba hiyo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
Jakaya Kikwete na Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein.
“Mimi naamini hata
ikibidi tupige kura zote mbili kwa wakati mmoja, ya kwanza ya kumchagua Rais na
nyingine ya kupitisha Katiba.
“Mama zangu nyie
nguvu yenu ni kubwa na tunaihitaji sana…mkijipanga vizuri na kutaka hili
lifanyike litafanikiwa hata bila nguvu yetu wanaume,” alisema Pinda.
Kauli hiyo ya Pinda,
inaweza kutafsiriwa vibaya kwamba anataka kukiuka makubaliano ya vyama vya
siasa na Rais Kikwete, ya kuahirisha mchakato wa Katiba ili Katiba iliyopo
irekebishwe kupisha kwanza Uchaguzi Mkuu.
Vyama hivyo vinataka
mchakato wa Katiba mpya ikiwezekana, uanze upya baada ya Uchaguzi Mkuu ujao
kumalizika na kupata Rais mpya wa Awamu ya Tano na wabunge.
Wakati huo huo, Pinda
amesema ili Katiba Inayopendekezwa iwafikishe Watanzania ilikokusudia, wananchi
wanatakiwa kukataa amani ya nchi kuchezewa.
Akizungumza baada ya
kupatikana kwa Katiba Inayopendekezwa jana bungeni, Pinda alisema wapo watu
ambao kila wakikaa wanawaza namna ya kuvuruga amani.
“Katika suala la
amani, nitaendelea kupigania nchi hii na kuilinda ili ndoto ya maendeleo kwa
Watanzania itimie,” alisema Pinda na kuelezea alivyofurahishwa na Sura ya Pili
ya Katiba hiyo.
Sura hiyo ya Pili,
imeweka malengo ya kitaifa, ambapo imeyagawa katika malengo ya kiuchumi,
kisiasa na kijamii na katika uchumi ikisisitiza Serikali kujenga ustawi sawia
wa Watanzania.
“Nimejifunza mengi na
kubwa nimeona watu tumekuwa na dhamira moja kwa umoja wetu na lengo moja la
kujenga Taifa moja,” alisema Pinda.
Alisema kabla ya
kupatikana kwa Katiba Inayopendekezwa, kila mjumbe alikuwa na hofu iwapo
theluthi mbili ya kura itapatikana na hasa upande wa Zanzibar, lakini
imepatikana.
“Sasa wale
waliotutakia mabaya sijui watasema nini,” alisema Pinda akishukuru wajumbe
kutoka Zanzibar kwa kumpa nguvu huku akimtaka Makamu wa Pili wa Rais wa
Zanzibar, Balozi Seif Ali Iddi, kupeleka salamu za shukrani kwa Rais wa
Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein.
Aliwataka Watanzania
wasome Katiba Inayopendekezwa, kwa kuwa ina mambo mazuri na kuongeza kuwa
imekamilika wakati mzuri ikiwa na malengo ya kiuchumi, wakati mwakani Serikali
ikiandaa mpango wa miaka mitano. Kwa mujibu wa Pinda, muda wote waliokaa Dodoma
kujadili Katiba hiyo, amejifunza kuwa Watanzania wanaweza kushindana kwa hoja
na kupingana bila kuachana na hivyo umoja wa nchi utaendelea kuimarika.
“Kwa nguvu hii
niliyoiona na umoja wetu kama tukitoka nao na kwenda kwa wananchi, hakuna
litakaloshindikana,” alisema.
Alisema amefuatilia
namna kila sehemu kulivyokuwa na mjadala wa nguvu, lakini mwishowe kukawa na
maridhiano, jambo lililodhihirisha kuwa sauti ya wengi ni ya Mungu.
“Mimi nimekaa pale
Ikulu mara zote mzee Kingunge (Ngombale Mwiru), amekuwa akiapa bila kushika
Bibilia wala Kurani, lakini leo kwa mara ya kwanza amesema tumshukuru Mungu,”
alisema Pinda.
Alisema kwa namna
walivyokuwa wakijadili na kupingana na jana wameikubali Katiba Inayopendekezwa
kwa pamoja, haamini kama kuna mtu anaweza kuipinga
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “ PINDA ATAMANI KURA KABLA YA UCHAGUZI MKUU .”
Post a Comment