Tuesday, August 16, 2016
HATIMAYE MZEE AKILIMALI AWEKA SIRAHA CHINI NA KUMUOMBA MSAMAHA MANJI.
Do you like this story?
Baada
ya wanachama wa klabu ya Yanga kumfuta uanachma mzee Akilimali Katibu wa baraza
la wazee Yanga, amejitokeza na kuomba radhi wanachama pamoja na mwenyekiti
Yusuph Manji huku akisema yeye ni mmoja wa watu wanaompenda sana Manji.
Akiongea
na Kituo cha Radio cha EFM jijini Dar es Salaam , Mzee Akilimali wakisemwa
"Hatuna tatizo na Manji tumeshamalizana na ataendelea kuwa mwenyekiti wa
Yanga mpaka pale atakapo amua kuacha mwenyewe"
Akiendelea
kuelezea alikiri kuwa chombo chenye maamuzi ndani ya klabu ya Yanga sio baraza
la wazee ambaye yeye ni Katibu wa baraza hilo bali ni baraza la wadhamini.
Hata
hivyo pamoja na Mzee Akilimali kuomba radhi bado kikao cha wenyeviti wa matawi
Kwa klabu ya Yanga wamepitisha pendekezo la kumsimamisha uanachama Mzee
Akilimali.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “HATIMAYE MZEE AKILIMALI AWEKA SIRAHA CHINI NA KUMUOMBA MSAMAHA MANJI.”
Post a Comment