Tuesday, August 16, 2016
JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LIMESEMA LIKO TAYARI KUTOA KIBALI KWA CHAMA CHOCHOTE CHA SIASA.
Do you like this story?
JESHI la polisi mkoani Mbeya limesema liko tayari
kutoa kibali kwa chama chochote cha siasa kinachotaka kufanya mikutano
ikiwa kitafuata sheria na taratibu za nchi.
Hayo
yamesemwa na Kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya, Dhahiri Kidavashari, wakati
alipokuwa akizungumza na Waandishi wa habari katika Ofisi za Kituo kikubwa cha
Polisi Mkoa wa Mbeya kuhusu matukio mbalimbali ya kiharifu yaliyotokea.
Amesema
kuwa vibali hivyo vitatolewa kulingana na mazingira ya wakati husika kwa madai
kuwa, hakuna utaratibu wa kufanya mikutano katika Wilaya zote kwa wakati mmoja.
Amesema
kuwa kwa mujibu wa Sheria, mikutano hiyo inahitaji ulinzi wa polisi kwa ajili
ya kulinda amani, hivyo akasema kuwa lazima vibali hivyo vizingatie hali
ya wakati huo.
“Haiwezekani
tukaruhusu maandamano katika Wilaya zote maana maandamano na mikutano hiyo
inahitaji ulinzi wa Jeshi la Polisi, sasa tukiruhusu vitu kama hivyo
tutashindwa kuweka ulinzi katika mikutano hiyo, kwa hiyo tutaangalia mtu
atakayefuata taratibu ndiye atakayeruhusiwa na kupewa ulinzi,” alisema
Kidavashari.
Amesema
kuwa yeyote atakayeomba kibali kwa mujibu wa taratibu ndiye atakaye pewa
ulinzi, lakini atakayekiuka atashughulikiwa kwa mujibu wa sheria.
Aliwataka wananchi kutokubali kurubuniwa na wanasiasa
ili kushiriki katika maandamano yaliyokatazwa kwa madai kuwa watashughulikiwa
na jeshi hilo kwa mujibu sheria zinavyotaka jeshi hilo kufanya.
Aliwataka
kuwa na uhakika na mikutano wanayohudhuria endapo inakuwa imeruhusiwa ama la,
ili wasijewakajikuta wanajiingiza katika matatizo.
Siku
za hivi karibuni Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kilitangaza kuwa
kufikia Septemba mosi mwaka huu kitafanya maandamano nchi nzima ili kupinga
kile walichokiita udikteta ambayo waliyabatiza jina la Ukuta.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
0 Responses to “JESHI LA POLISI MKOA WA MBEYA LIMESEMA LIKO TAYARI KUTOA KIBALI KWA CHAMA CHOCHOTE CHA SIASA.”
Post a Comment